Sura Al-Balad
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Balad pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Balad pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Balad Tafsiri. Al-Balad (Makka) 20 Aya.
Related
- Al-Balad TafsiriKiswahili
- Al-Balad mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Balad

ﭽﭾﭿﮀﮁ
Naapa kwa Mji huu!
ﮂﮃﮄﮅﮆ
Nawe unaukaa Mji huu.
ﮇﮈﮉﮊ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
ﮘﮙﮚﮛﮜ
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
ﮣﮤﮥﮦﮧ
Kwani hatukumpa macho mawili?
ﮨﮩﮪ
Na ulimi, na midomo miwili?
ﮫﮬﮭ
Na tukambainishia zote njia mbili?
ﮮﮯﮰﮱ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
ﯘﯙﯚ
Kumkomboa mtumwa;
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Au kumlisha siku ya njaa
ﯢﯣﯤﯥ
Yatima aliye jamaa,
ﯦﯧﯨﯩﯪ
Au masikini aliye vumbini.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
ﯵﯶﯷﯸ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
ﭘﭙﭚﭛ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







