Sura Al-Balad pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Balad pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Balad Tafsiri. Sura Al-Balad (Makka) 20 Aya.
Related
- Sura Al-Balad TafsiriKiswahili
- Sura Al-Balad mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Balad

ﭽﭾﭿﮀﮁ
90:1
Naapa kwa Mji huu!
ﮂﮃﮄﮅﮆ
90:2
Nawe unaukaa Mji huu.
ﮇﮈﮉﮊ
90:3
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
90:4
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
90:5
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
ﮘﮙﮚﮛﮜ
90:6
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
90:7
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
ﮣﮤﮥﮦﮧ
90:8
Kwani hatukumpa macho mawili?
ﮨﮩﮪ
90:9
Na ulimi, na midomo miwili?
ﮫﮬﮭ
90:10
Na tukambainishia zote njia mbili?
ﮮﮯﮰﮱ
90:11
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
90:12
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
ﯘﯙﯚ
90:13
Kumkomboa mtumwa;
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
90:14
Au kumlisha siku ya njaa
ﯢﯣﯤﯥ
90:15
Yatima aliye jamaa,
ﯦﯧﯨﯩﯪ
90:16
Au masikini aliye vumbini.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
90:17
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
ﯵﯶﯷﯸ
90:18
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
90:19
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
ﭘﭙﭚﭛ
90:20
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







