Sura Ash-Shams pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Ash-Shams pdf Kiswahili — Pakua Sura Ash-Shams Tafsiri. Sura Ash-Shams (Makka) 15 Aya.
Related
- Sura Ash-Shams TafsiriKiswahili
- Sura Ash-Shams mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Ash-Shams

ﭜﭝﭞ
91:1
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
ﭟﭠﭡﭢ
91:2
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
ﭣﭤﭥﭦ
91:3
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
ﭧﭨﭩﭪ
91:4
Na kwa usiku unapo lifunika!
ﭫﭬﭭﭮ
91:5
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
ﭯﭰﭱﭲ
91:6
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
ﭳﭴﭵﭶ
91:7
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
ﭷﭸﭹﭺ
91:8
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
ﭻﭼﭽﭾﭿ
91:9
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
ﮀﮁﮂﮃﮄ
91:10
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
ﮅﮆﮇﮈ
91:11
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
ﮉﮊﮋﮌ
91:12
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
91:13
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
91:14
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
ﮝﮞﮟﮠ
91:15
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







