Sura At-Tur kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura At-Tur na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (49 Aya — مكية). At-Tur Sikiliza, At-Tur Tafsiri, At-Tur mp3, At-Tur pdf.

Soma na Sikiliza Sura At-Tur

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
وَالطُّورِ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Naapa kwa mlima wa T'ur,
وَكِتَابٍ مَّسْطُورٍ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Na Kitabu kilicho andikwa
فِي رَقٍّ مَّنشُورٍ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
وَالْبَيْتِ الْمَعْمُورِ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
وَالسَّقْفِ الْمَرْفُوعِ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
وَالْبَحْرِ الْمَسْجُورِ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Na kwa bahari iliyo jazwa,
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَاقِعٌ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
مَّا لَهُ مِن دَافِعٍ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Hapana wa kuizuia.
يَوْمَ تَمُورُ السَّمَاءُ مَوْرًا ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
وَتَسِيرُ الْجِبَالُ سَيْرًا ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
فَوَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
الَّذِينَ هُمْ فِي خَوْضٍ يَلْعَبُونَ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
هَٰذِهِ النَّارُ الَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
أَفَسِحْرٌ هَٰذَا أَمْ أَنتُمْ لَا تُبْصِرُونَ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
اصْلَوْهَا فَاصْبِرُوا أَوْ لَا تَصْبِرُوا سَوَاءٌ عَلَيْكُمْ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَعِيمٍ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
فَاكِهِينَ بِمَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَاهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ سُرُرٍ مَّصْفُوفَةٍ ۖ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَاتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَانٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَا أَلَتْنَاهُم مِّنْ عَمَلِهِم مِّن شَيْءٍ ۚ كُلُّ امْرِئٍ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
وَأَمْدَدْنَاهُم بِفَاكِهَةٍ وَلَحْمٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
يَتَنَازَعُونَ فِيهَا كَأْسًا لَّا لَغْوٌ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
۞ وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌ لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌ مَّكْنُونٌ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Wataelekeana wakiulizana.
قَالُوا إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِي أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
فَمَنَّ اللَّهُ عَلَيْنَا وَوَقَانَا عَذَابَ السَّمُومِ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
فَذَكِّرْ فَمَا أَنتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍ وَلَا مَجْنُونٍ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌ نَّتَرَبَّصُ بِهِ رَيْبَ الْمَنُونِ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
قُلْ تَرَبَّصُوا فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ الْمُتَرَبِّصِينَ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلَامُهُم بِهَٰذَا ۚ أَمْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُ ۚ بَل لَّا يُؤْمِنُونَ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
فَلْيَأْتُوا بِحَدِيثٍ مِّثْلِهِ إِن كَانُوا صَادِقِينَ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
أَمْ خُلِقُوا مِنْ غَيْرِ شَيْءٍ أَمْ هُمُ الْخَالِقُونَ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
أَمْ خَلَقُوا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
أَمْ عِندَهُمْ خَزَائِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ الْمُصَيْطِرُونَ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
أَمْ لَهُمْ سُلَّمٌ يَسْتَمِعُونَ فِيهِ ۖ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
أَمْ لَهُ الْبَنَاتُ وَلَكُمُ الْبَنُونَ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدًا ۖ فَالَّذِينَ كَفَرُوا هُمُ الْمَكِيدُونَ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
أَمْ لَهُمْ إِلَٰهٌ غَيْرُ اللَّهِ ۚ سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
وَإِن يَرَوْا كِسْفًا مِّنَ السَّمَاءِ سَاقِطًا يَقُولُوا سَحَابٌ مَّرْكُومٌ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
فَذَرْهُمْ حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي فِيهِ يُصْعَقُونَ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
يَوْمَ لَا يُغْنِي عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا عَذَابًا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
وَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا ۖ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
وَمِنَ اللَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَارَ النُّجُومِ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
← 51 At-Tur (52/114) 53 →
Soma Sura At-Tur kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

52الطور At-Tur 📚 49 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema