Sura Ash-Shu'ara
PDF —
227 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Ash-Shu'ara pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Ash-Shu'ara pdf Kiswahili — Pakua Sura Ash-Shu'ara Tafsiri. Ash-Shu'ara (Makka) 227 Aya.



Sura Ash-Shu'ara
227 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒ
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
ﭓﭔﭕﭖﭗ
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
ﯼﯽﯾﯿﰀ
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
ﮈﮉﮊﮋ
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
ﮌﮍﮎﮏﮐ
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮑﮒﮓﮔ
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
ﯳﯴﯵﯶﯷ
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
ﯸﯹﯺﯻ
Nao wanatuudhi.
ﯼﯽﯾﯿ
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
ﰀﰁﰂﰃﰄ
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
ﰅﰆﰇﰈ
Na makhazina, na vyeo vya hishima,
ﰉﰊﰋﰌﰍﰎ
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
ﰏﰐﰑ
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
ﭱﭲﭳﭴ
Na tukawajongeza hapo wale wengine.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
ﭻﭼﭽﭾ
Kisha tukawazamisha hao wengine.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮏﮐﮑﮒﮓ
Na wasomee khabari za Ibrahim.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
ﮨﮩﮪﮫﮬ
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
ﯛﯜﯝﯞ
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﯦﯧﯨﯩﯪ
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
ﯫﯬﯭﯮﯯ
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
ﯰﯱﯲﯳﯴ
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
ﯵﯶﯷﯸﯹ
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
ﭸﭹﭺﭻ
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
ﭼﭽﭾﭿ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
ﮏﮐﮑﮒﮓ
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
ﮔﮕﮖﮗ
Na majeshi ya Ibilisi yote.
ﮘﮙﮚﮛﮜ
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
ﮤﮥﮦﮧﮨ
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
ﮮﮯﮰﮱﯓ
Basi hatuna waombezi.
ﯔﯕﯖﯗ
Wala rafiki wa dhati.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﯰﯱﯲﯳﯴ
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
ﯽﯾﯿﰀﰁ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﰂﰃﰄﰅ
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒ
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﰓﰔﰕﰖ
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﰗﰘﰙﰚﰛﰜﰝ
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
ﭡﭢﭣﭤﭥ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
ﮌﮍﮎﮏﮐ
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮡﮢﮣﮤ
Kina A'd waliwakanusha Mitume.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
ﮭﮮﮯﮰﮱ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﯓﯔﯕﯖ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
ﯪﯫﯬﯭﯮ
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
ﯯﯰﯱﯲﯳ
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
ﯴﯵﯶﯷ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
ﯾﯿﰀﰁ
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.
ﰂﰃﰄ
Na mabustani na chemchem.
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
ﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
ﭗﭘﭙﭚ
Wala sisi hatutaadhibiwa.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﭮﭯﭰﭱ
Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
ﭺﭻﭼﭽﭾ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﭿﮀﮁﮂ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
ﮖﮗﮘﮙ
Katika mabustani, na chemchem?
ﮚﮛﮜﮝﮞ
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
ﮥﮦﮧﮨ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
ﯺﯻﯼﯽ
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
ﭞﭟﭠﭡﭢ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
ﭣﭤﭥﭦ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﭴﭵﭶﭷﭸ
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
ﮛﮜﮝﮞ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
ﮟﮠﮡﮢﮣ
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
ﮤﮥﮦﮧ
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
ﯡﯢﯣﯤﯥ
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
ﯭﯮﯯﯰﯱ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﯲﯳﯴﯵ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
ﰋﰌﰍﰎ
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;
ﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘ
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮓﮔﮕﮖﮗ
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮘﮙﮚﮛﮜ
Ameuteremsha Roho muaminifu,
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
ﮣﮤﮥﮦ
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
ﮧﮨﮩﮪﮫ
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
ﯸﯹﯺﯻﯼ
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
ﯽﯾﯿ
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?
ﰀﰁﰂﰃﰄ
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -
ﭠﭡﭢﭣﭤ
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
ﭰﭱﭲﭳﭴ
Hakika hao wametengwa na kusikia.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
ﭿﮀﮁﮂ
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
ﮒﮓﮔﮕﮖ
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮗﮘﮙﮚﮛ
Ambaye anakuona unapo simama,
ﮜﮝﮞﮟ
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.
ﮠﮡﮢﮣﮤ
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
ﯘﯙﯚﯛ
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema