Sura Ash-Shu'ara pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Ash-Shu'ara pdf Kiswahili — Pakua Sura Ash-Shu'ara Tafsiri. Sura Ash-Shu'ara (Makka) 227 Aya.
Related
- Sura Ash-Shu'ara TafsiriKiswahili
- Sura Ash-Shu'ara mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Ash-Shu'ara

ﭑﭒ
26:1
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
ﭓﭔﭕﭖﭗ
26:2
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
26:3
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
26:4
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
26:5
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
26:6
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
26:7
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
26:8
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
26:9
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
26:10
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
26:11
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
26:12
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
26:13
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
26:14
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
26:15
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
26:16
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
26:17
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
26:18
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
26:19
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
26:20
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
26:21
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
26:22
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
26:23
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
26:24
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
26:25
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
26:26
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
26:27
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
26:28
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
26:29
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
26:30
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
26:31
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
26:32
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
26:33
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
26:34
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
26:35
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
26:36
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
ﯼﯽﯾﯿﰀ
26:37
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
26:38
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
26:39
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
26:40
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
26:41
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
26:42
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
26:43
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
26:44
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
26:45
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
ﮈﮉﮊﮋ
26:46
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
ﮌﮍﮎﮏﮐ
26:47
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮑﮒﮓﮔ
26:48
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
26:49
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
26:50
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
26:51
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
26:52
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
26:53
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
ﯳﯴﯵﯶﯷ
26:54
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
ﯸﯹﯺﯻ
26:55
Nao wanatuudhi.
ﯼﯽﯾﯿ
26:56
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
ﰀﰁﰂﰃﰄ
26:57
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
ﰅﰆﰇﰈ
26:58
Na makhazina, na vyeo vya hishima,
ﰉﰊﰋﰌﰍﰎ
26:59
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
ﰏﰐﰑ
26:60
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
26:61
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
26:62
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
26:63
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
ﭱﭲﭳﭴ
26:64
Na tukawajongeza hapo wale wengine.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
26:65
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
ﭻﭼﭽﭾ
26:66
Kisha tukawazamisha hao wengine.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
26:67
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
26:68
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮏﮐﮑﮒﮓ
26:69
Na wasomee khabari za Ibrahim.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
26:70
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
26:71
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
26:72
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
ﮨﮩﮪﮫﮬ
26:73
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
26:74
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
26:75
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
ﯛﯜﯝﯞ
26:76
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
26:77
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﯦﯧﯨﯩﯪ
26:78
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
ﯫﯬﯭﯮﯯ
26:79
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
ﯰﯱﯲﯳﯴ
26:80
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
ﯵﯶﯷﯸﯹ
26:81
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
26:82
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
26:83
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
26:84
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
26:85
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
26:86
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
26:87
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
26:88
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
26:89
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
ﭸﭹﭺﭻ
26:90
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
ﭼﭽﭾﭿ
26:91
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
26:92
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
26:93
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
ﮏﮐﮑﮒﮓ
26:94
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
ﮔﮕﮖﮗ
26:95
Na majeshi ya Ibilisi yote.
ﮘﮙﮚﮛﮜ
26:96
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
26:97
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
ﮤﮥﮦﮧﮨ
26:98
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
26:99
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
ﮮﮯﮰﮱﯓ
26:100
Basi hatuna waombezi.
ﯔﯕﯖﯗ
26:101
Wala rafiki wa dhati.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
26:102
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
26:103
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
26:104
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﯰﯱﯲﯳﯴ
26:105
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
26:106
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
ﯽﯾﯿﰀﰁ
26:107
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﰂﰃﰄﰅ
26:108
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒ
26:109
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﰓﰔﰕﰖ
26:110
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﰗﰘﰙﰚﰛﰜﰝ
26:111
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
26:112
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
26:113
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
ﭡﭢﭣﭤﭥ
26:114
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
26:115
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
26:116
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
26:117
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
26:118
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
26:119
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
ﮌﮍﮎﮏﮐ
26:120
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
26:121
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
26:122
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮡﮢﮣﮤ
26:123
Kina A'd waliwakanusha Mitume.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
26:124
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
ﮭﮮﮯﮰﮱ
26:125
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﯓﯔﯕﯖ
26:126
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
26:127
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
26:128
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
ﯪﯫﯬﯭﯮ
26:129
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
ﯯﯰﯱﯲﯳ
26:130
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
ﯴﯵﯶﯷ
26:131
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
26:132
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
ﯾﯿﰀﰁ
26:133
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.
ﰂﰃﰄ
26:134
Na mabustani na chemchem.
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
26:135
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
ﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
26:136
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
26:137
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
ﭗﭘﭙﭚ
26:138
Wala sisi hatutaadhibiwa.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
26:139
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
26:140
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﭮﭯﭰﭱ
26:141
Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
26:142
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
ﭺﭻﭼﭽﭾ
26:143
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﭿﮀﮁﮂ
26:144
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
26:145
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
26:146
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
ﮖﮗﮘﮙ
26:147
Katika mabustani, na chemchem?
ﮚﮛﮜﮝﮞ
26:148
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
26:149
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
ﮥﮦﮧﮨ
26:150
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
26:151
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
26:152
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
26:153
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
26:154
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
26:155
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
26:156
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
ﯺﯻﯼﯽ
26:157
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
26:158
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
26:159
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
26:160
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
26:161
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
ﭞﭟﭠﭡﭢ
26:162
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
ﭣﭤﭥﭦ
26:163
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
26:164
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﭴﭵﭶﭷﭸ
26:165
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
26:166
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
26:167
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
26:168
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
26:169
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
ﮛﮜﮝﮞ
26:170
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
ﮟﮠﮡﮢﮣ
26:171
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
ﮤﮥﮦﮧ
26:172
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
26:173
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
26:174
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
26:175
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
ﯡﯢﯣﯤﯥ
26:176
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
26:177
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
ﯭﯮﯯﯰﯱ
26:178
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ﯲﯳﯴﯵ
26:179
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
26:180
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
26:181
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
ﰋﰌﰍﰎ
26:182
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;
ﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘ
26:183
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
26:184
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
26:185
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
26:186
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
26:187
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
26:188
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
26:189
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
26:190
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
26:191
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮓﮔﮕﮖﮗ
26:192
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮘﮙﮚﮛﮜ
26:193
Ameuteremsha Roho muaminifu,
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
26:194
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
ﮣﮤﮥﮦ
26:195
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
ﮧﮨﮩﮪﮫ
26:196
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
26:197
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
26:198
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
26:199
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
26:200
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
26:201
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
26:202
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
ﯸﯹﯺﯻﯼ
26:203
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
ﯽﯾﯿ
26:204
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?
ﰀﰁﰂﰃﰄ
26:205
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
26:206
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
26:207
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
26:208
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -
ﭠﭡﭢﭣﭤ
26:209
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
26:210
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
26:211
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
ﭰﭱﭲﭳﭴ
26:212
Hakika hao wametengwa na kusikia.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
26:213
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
ﭿﮀﮁﮂ
26:214
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
26:215
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
26:216
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
ﮒﮓﮔﮕﮖ
26:217
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
ﮗﮘﮙﮚﮛ
26:218
Ambaye anakuona unapo simama,
ﮜﮝﮞﮟ
26:219
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.
ﮠﮡﮢﮣﮤ
26:220
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
26:221
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
26:222
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
26:223
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
ﯘﯙﯚﯛ
26:224
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
26:225
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
26:226
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
26:227
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







