Sura Ash-Shu'ara kwa Kiarabu na Kiswahili
Soma Sura Ash-Shu'ara na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (227 Aya — مكية). Ash-Shu'ara Sikiliza, Ash-Shu'ara Tafsiri, Ash-Shu'ara mp3, Ash-Shu'ara pdf.Soma na Sikiliza Sura Ash-Shu'ara
🎧 Aya
M
Mishary Rashid Alafasy
✓
Mishary Rashid Alafasy
✓
M
Mahmoud Khalil Al-Husary
✓
Mahmoud Khalil Al-Husary
✓
A
Abdurrahman As-Sudais
✓
Abdurrahman As-Sudais
✓
M
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
✓
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
✓
A
Abdul Basit Abdul Samad
✓
Abdul Basit Abdul Samad
✓
A
Ali Al-Hudhaify
✓
Ali Al-Hudhaify
✓
A
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
✓
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
✓
A
Abu Bakr Ash-Shaatree
✓
Abu Bakr Ash-Shaatree
✓
M
Muhammad Ayyoub
✓
Muhammad Ayyoub
✓
A
Abdullah Basfar
✓
Abdullah Basfar
✓
A
Abdullah Al-Juhani
✓
Abdullah Al-Juhani
✓
M
Maher Al Muaiqly
✓
Maher Al Muaiqly
✓
—
x1
لَعَلَّكَ بَاخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا مُؤْمِنِينَ ٣
📖 Tafsiri
Aya 3
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ السَّمَاءِ آيَةً فَظَلَّتْ أَعْنَاقُهُمْ لَهَا خَاضِعِينَ ٤
📖 Tafsiri
Aya 4
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ الرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا عَنْهُ مُعْرِضِينَ ٥
📖 Tafsiri
Aya 5
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
فَقَدْ كَذَّبُوا فَسَيَأْتِيهِمْ أَنبَاءُ مَا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ ٦
📖 Tafsiri
Aya 6
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الْأَرْضِ كَمْ أَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ ٧
📖 Tafsiri
Aya 7
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ٨
📖 Tafsiri
Aya 8
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ٩
📖 Tafsiri
Aya 9
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰ أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ ١٠
📖 Tafsiri
Aya 10
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
قَالَ رَبِّ إِنِّي أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ ١٢
📖 Tafsiri
Aya 12
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
وَيَضِيقُ صَدْرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَارُونَ ١٣
📖 Tafsiri
Aya 13
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
وَلَهُمْ عَلَيَّ ذَنبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ ١٤
📖 Tafsiri
Aya 14
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
قَالَ كَلَّا ۖ فَاذْهَبَا بِآيَاتِنَا ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ ١٥
📖 Tafsiri
Aya 15
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَا إِنَّا رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٦
📖 Tafsiri
Aya 16
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ ١٨
📖 Tafsiri
Aya 18
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ الَّتِي فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ الْكَافِرِينَ ١٩
📖 Tafsiri
Aya 19
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
قَالَ فَعَلْتُهَا إِذًا وَأَنَا مِنَ الضَّالِّينَ ٢٠
📖 Tafsiri
Aya 20
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكْمًا وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُرْسَلِينَ ٢١
📖 Tafsiri
Aya 21
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِي إِسْرَائِيلَ ٢٢
📖 Tafsiri
Aya 22
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ الْعَالَمِينَ ٢٣
📖 Tafsiri
Aya 23
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
قَالَ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ ٢٤
📖 Tafsiri
Aya 24
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُ أَلَا تَسْتَمِعُونَ ٢٥
📖 Tafsiri
Aya 25
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ ٢٦
📖 Tafsiri
Aya 26
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ الَّذِي أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ ٢٧
📖 Tafsiri
Aya 27
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
قَالَ رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ ٢٨
📖 Tafsiri
Aya 28
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
قَالَ لَئِنِ اتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِي لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ الْمَسْجُونِينَ ٢٩
📖 Tafsiri
Aya 29
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَيْءٍ مُّبِينٍ ٣٠
📖 Tafsiri
Aya 30
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
قَالَ فَأْتِ بِهِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ٣١
📖 Tafsiri
Aya 31
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ ٣٢
📖 Tafsiri
Aya 32
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
وَنَزَعَ يَدَهُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ ٣٣
📖 Tafsiri
Aya 33
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُ إِنَّ هَٰذَا لَسَاحِرٌ عَلِيمٌ ٣٤
📖 Tafsiri
Aya 34
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ ٣٥
📖 Tafsiri
Aya 35
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
قَالُوا أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَابْعَثْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ ٣٦
📖 Tafsiri
Aya 36
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
فَجُمِعَ السَّحَرَةُ لِمِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ ٣٨
📖 Tafsiri
Aya 38
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ ٣٩
📖 Tafsiri
Aya 39
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ السَّحَرَةَ إِن كَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ ٤٠
📖 Tafsiri
Aya 40
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
فَلَمَّا جَاءَ السَّحَرَةُ قَالُوا لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ ٤١
📖 Tafsiri
Aya 41
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ الْمُقَرَّبِينَ ٤٢
📖 Tafsiri
Aya 42
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ أَلْقُوا مَا أَنتُم مُّلْقُونَ ٤٣
📖 Tafsiri
Aya 43
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ ٤٤
📖 Tafsiri
Aya 44
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ ٤٥
📖 Tafsiri
Aya 45
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ٤٧
📖 Tafsiri
Aya 47
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
قَالَ آمَنتُمْ لَهُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ ٤٩
📖 Tafsiri
Aya 49
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
قَالُوا لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ ٥٠
📖 Tafsiri
Aya 50
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَن كُنَّا أَوَّلَ الْمُؤْمِنِينَ ٥١
📖 Tafsiri
Aya 51
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
۞ وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِي إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ ٥٢
📖 Tafsiri
Aya 52
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ ٥٣
📖 Tafsiri
Aya 53
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ ٥٤
📖 Tafsiri
Aya 54
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
فَأَخْرَجْنَاهُم مِّن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ٥٧
📖 Tafsiri
Aya 57
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا بَنِي إِسْرَائِيلَ ٥٩
📖 Tafsiri
Aya 59
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَىٰ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ ٦١
📖 Tafsiri
Aya 61
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
قَالَ كَلَّا ۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ ٦٢
📖 Tafsiri
Aya 62
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْبَحْرَ ۖ فَانفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ ٦٣
📖 Tafsiri
Aya 63
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَجْمَعِينَ ٦٥
📖 Tafsiri
Aya 65
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ٦٧
📖 Tafsiri
Aya 67
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ٦٨
📖 Tafsiri
Aya 68
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَا تَعْبُدُونَ ٧٠
📖 Tafsiri
Aya 70
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
قَالُوا نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَاكِفِينَ ٧١
📖 Tafsiri
Aya 71
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ ٧٢
📖 Tafsiri
Aya 72
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
قَالُوا بَلْ وَجَدْنَا آبَاءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ ٧٤
📖 Tafsiri
Aya 74
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّي إِلَّا رَبَّ الْعَالَمِينَ ٧٧
📖 Tafsiri
Aya 77
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
الَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهْدِينِ ٧٨
📖 Tafsiri
Aya 78
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
وَالَّذِي هُوَ يُطْعِمُنِي وَيَسْقِينِ ٧٩
📖 Tafsiri
Aya 79
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ ٨٠
📖 Tafsiri
Aya 80
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
وَالَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحْيِينِ ٨١
📖 Tafsiri
Aya 81
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
وَالَّذِي أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِي خَطِيئَتِي يَوْمَ الدِّينِ ٨٢
📖 Tafsiri
Aya 82
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
رَبِّ هَبْ لِي حُكْمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ ٨٣
📖 Tafsiri
Aya 83
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
وَاجْعَل لِّي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الْآخِرِينَ ٨٤
📖 Tafsiri
Aya 84
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
وَاجْعَلْنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ ٨٥
📖 Tafsiri
Aya 85
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّهُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ ٨٦
📖 Tafsiri
Aya 86
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ٨٨
📖 Tafsiri
Aya 88
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ٨٩
📖 Tafsiri
Aya 89
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ ٩٢
📖 Tafsiri
Aya 92
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
مِن دُونِ اللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ ٩٣
📖 Tafsiri
Aya 93
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ ٩٤
📖 Tafsiri
Aya 94
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
تَاللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ٩٧
📖 Tafsiri
Aya 97
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ٩٨
📖 Tafsiri
Aya 98
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ١٠٢
📖 Tafsiri
Aya 102
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ١٠٣
📖 Tafsiri
Aya 103
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ١٠٤
📖 Tafsiri
Aya 104
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ ١٠٦
📖 Tafsiri
Aya 106
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ ١٠٨
📖 Tafsiri
Aya 108
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٠٩
📖 Tafsiri
Aya 109
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ ١١٠
📖 Tafsiri
Aya 110
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
۞ قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ ١١١
📖 Tafsiri
Aya 111
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ١١٢
📖 Tafsiri
Aya 112
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ ١١٣
📖 Tafsiri
Aya 113
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ ١١٥
📖 Tafsiri
Aya 115
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ ١١٦
📖 Tafsiri
Aya 116
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ ١١٧
📖 Tafsiri
Aya 117
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ١١٨
📖 Tafsiri
Aya 118
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
فَأَنجَيْنَاهُ وَمَن مَّعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ١١٩
📖 Tafsiri
Aya 119
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ ١٢٠
📖 Tafsiri
Aya 120
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ١٢١
📖 Tafsiri
Aya 121
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ١٢٢
📖 Tafsiri
Aya 122
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ ١٢٤
📖 Tafsiri
Aya 124
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ ١٢٦
📖 Tafsiri
Aya 126
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٢٧
📖 Tafsiri
Aya 127
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ آيَةً تَعْبَثُونَ ١٢٨
📖 Tafsiri
Aya 128
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ ١٢٩
📖 Tafsiri
Aya 129
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ ١٣٠
📖 Tafsiri
Aya 130
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
وَاتَّقُوا الَّذِي أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ ١٣٢
📖 Tafsiri
Aya 132
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ١٣٥
📖 Tafsiri
Aya 135
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
قَالُوا سَوَاءٌ عَلَيْنَا أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ الْوَاعِظِينَ ١٣٦
📖 Tafsiri
Aya 136
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
إِنْ هَٰذَا إِلَّا خُلُقُ الْأَوَّلِينَ ١٣٧
📖 Tafsiri
Aya 137
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَاهُمْ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ١٣٩
📖 Tafsiri
Aya 139
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ١٤٠
📖 Tafsiri
Aya 140
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَالِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ ١٤٢
📖 Tafsiri
Aya 142
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٤٥
📖 Tafsiri
Aya 145
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَتُتْرَكُونَ فِي مَا هَاهُنَا آمِنِينَ ١٤٦
📖 Tafsiri
Aya 146
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ ١٤٨
📖 Tafsiri
Aya 148
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
وَتَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا فَارِهِينَ ١٤٩
📖 Tafsiri
Aya 149
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ ١٥٠
📖 Tafsiri
Aya 150
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَلَا تُطِيعُوا أَمْرَ الْمُسْرِفِينَ ١٥١
📖 Tafsiri
Aya 151
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
الَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ ١٥٢
📖 Tafsiri
Aya 152
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ ١٥٣
📖 Tafsiri
Aya 153
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
مَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِآيَةٍ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ١٥٤
📖 Tafsiri
Aya 154
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
قَالَ هَٰذِهِ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ ١٥٥
📖 Tafsiri
Aya 155
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ ١٥٦
📖 Tafsiri
Aya 156
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا نَادِمِينَ ١٥٧
📖 Tafsiri
Aya 157
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
فَأَخَذَهُمُ الْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ١٥٨
📖 Tafsiri
Aya 158
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ١٥٩
📖 Tafsiri
Aya 159
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ ١٦١
📖 Tafsiri
Aya 161
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٦٤
📖 Tafsiri
Aya 164
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَتَأْتُونَ الذُّكْرَانَ مِنَ الْعَالَمِينَ ١٦٥
📖 Tafsiri
Aya 165
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَاجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ ١٦٦
📖 Tafsiri
Aya 166
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا لُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمُخْرَجِينَ ١٦٧
📖 Tafsiri
Aya 167
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ الْقَالِينَ ١٦٨
📖 Tafsiri
Aya 168
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
رَبِّ نَجِّنِي وَأَهْلِي مِمَّا يَعْمَلُونَ ١٦٩
📖 Tafsiri
Aya 169
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
فَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ ١٧٠
📖 Tafsiri
Aya 170
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ ١٧١
📖 Tafsiri
Aya 171
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَاءَ مَطَرُ الْمُنذَرِينَ ١٧٣
📖 Tafsiri
Aya 173
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ١٧٤
📖 Tafsiri
Aya 174
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ١٧٥
📖 Tafsiri
Aya 175
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
كَذَّبَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ الْمُرْسَلِينَ ١٧٦
📖 Tafsiri
Aya 176
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ ١٧٧
📖 Tafsiri
Aya 177
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
فَاتَّقُوا اللَّهَ وَأَطِيعُونِ ١٧٩
📖 Tafsiri
Aya 179
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٨٠
📖 Tafsiri
Aya 180
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
۞ أَوْفُوا الْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا مِنَ الْمُخْسِرِينَ ١٨١
📖 Tafsiri
Aya 181
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ ١٨٣
📖 Tafsiri
Aya 183
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
وَاتَّقُوا الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالْجِبِلَّةَ الْأَوَّلِينَ ١٨٤
📖 Tafsiri
Aya 184
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ ١٨٥
📖 Tafsiri
Aya 185
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
وَمَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ الْكَاذِبِينَ ١٨٦
📖 Tafsiri
Aya 186
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ١٨٧
📖 Tafsiri
Aya 187
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
قَالَ رَبِّي أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ ١٨٨
📖 Tafsiri
Aya 188
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ الظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ١٨٩
📖 Tafsiri
Aya 189
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ١٩٠
📖 Tafsiri
Aya 190
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ١٩١
📖 Tafsiri
Aya 191
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
وَإِنَّهُ لَتَنزِيلُ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٩٢
📖 Tafsiri
Aya 192
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ الْمُنذِرِينَ ١٩٤
📖 Tafsiri
Aya 194
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
وَإِنَّهُ لَفِي زُبُرِ الْأَوَّلِينَ ١٩٦
📖 Tafsiri
Aya 196
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ آيَةً أَن يَعْلَمَهُ عُلَمَاءُ بَنِي إِسْرَائِيلَ ١٩٧
📖 Tafsiri
Aya 197
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
وَلَوْ نَزَّلْنَاهُ عَلَىٰ بَعْضِ الْأَعْجَمِينَ ١٩٨
📖 Tafsiri
Aya 198
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
فَقَرَأَهُ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا بِهِ مُؤْمِنِينَ ١٩٩
📖 Tafsiri
Aya 199
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
كَذَٰلِكَ سَلَكْنَاهُ فِي قُلُوبِ الْمُجْرِمِينَ ٢٠٠
📖 Tafsiri
Aya 200
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِ حَتَّىٰ يَرَوُا الْعَذَابَ الْأَلِيمَ ٢٠١
📖 Tafsiri
Aya 201
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ٢٠٢
📖 Tafsiri
Aya 202
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
أَفَرَأَيْتَ إِن مَّتَّعْنَاهُمْ سِنِينَ ٢٠٥
📖 Tafsiri
Aya 205
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
ثُمَّ جَاءَهُم مَّا كَانُوا يُوعَدُونَ ٢٠٦
📖 Tafsiri
Aya 206
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
مَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يُمَتَّعُونَ ٢٠٧
📖 Tafsiri
Aya 207
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
وَمَا أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ ٢٠٨
📖 Tafsiri
Aya 208
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -
ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَالِمِينَ ٢٠٩
📖 Tafsiri
Aya 209
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ ٢١١
📖 Tafsiri
Aya 211
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
فَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّهِ إِلَٰهًا آخَرَ فَتَكُونَ مِنَ الْمُعَذَّبِينَ ٢١٣
📖 Tafsiri
Aya 213
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ٢١٤
📖 Tafsiri
Aya 214
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ٢١٥
📖 Tafsiri
Aya 215
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّي بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ ٢١٦
📖 Tafsiri
Aya 216
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
وَتَوَكَّلْ عَلَى الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ ٢١٧
📖 Tafsiri
Aya 217
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ٢٢٠
📖 Tafsiri
Aya 220
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ الشَّيَاطِينُ ٢٢١
📖 Tafsiri
Aya 221
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ ٢٢٢
📖 Tafsiri
Aya 222
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
يُلْقُونَ السَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَاذِبُونَ ٢٢٣
📖 Tafsiri
Aya 223
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
وَالشُّعَرَاءُ يَتَّبِعُهُمُ الْغَاوُونَ ٢٢٤
📖 Tafsiri
Aya 224
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِي كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ ٢٢٥
📖 Tafsiri
Aya 225
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ ٢٢٦
📖 Tafsiri
Aya 226
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَذَكَرُوا اللَّهَ كَثِيرًا وَانتَصَرُوا مِن بَعْدِ مَا ظُلِمُوا ۗ وَسَيَعْلَمُ الَّذِينَ ظَلَمُوا أَيَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ ٢٢٧
📖 Tafsiri
Aya 227
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
Soma Sura Ash-Shu'ara kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema

