Sura Al-Haqqa kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Al-Haqqa na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (52 Aya — مكية). Al-Haqqa Sikiliza, Al-Haqqa Tafsiri, Al-Haqqa mp3, Al-Haqqa pdf.

Soma na Sikiliza Sura Al-Haqqa

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
الْحَاقَّةُ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Tukio la haki.
مَا الْحَاقَّةُ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Nini hilo Tukio la haki?
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْحَاقَّةُ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
كَذَّبَتْ ثَمُودُ وَعَادٌ بِالْقَارِعَةِ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهْلِكُوا بِالطَّاغِيَةِ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
وَأَمَّا عَادٌ فَأُهْلِكُوا بِرِيحٍ صَرْصَرٍ عَاتِيَةٍ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
سَخَّرَهَا عَلَيْهِمْ سَبْعَ لَيَالٍ وَثَمَانِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومًا فَتَرَى الْقَوْمَ فِيهَا صَرْعَىٰ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ خَاوِيَةٍ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
فَهَلْ تَرَىٰ لَهُم مِّن بَاقِيَةٍ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
وَجَاءَ فِرْعَوْنُ وَمَن قَبْلَهُ وَالْمُؤْتَفِكَاتُ بِالْخَاطِئَةِ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
فَعَصَوْا رَسُولَ رَبِّهِمْ فَأَخَذَهُمْ أَخْذَةً رَّابِيَةً ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
إِنَّا لَمَّا طَغَى الْمَاءُ حَمَلْنَاكُمْ فِي الْجَارِيَةِ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
لِنَجْعَلَهَا لَكُمْ تَذْكِرَةً وَتَعِيَهَا أُذُنٌ وَاعِيَةٌ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ نَفْخَةٌ وَاحِدَةٌ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
وَحُمِلَتِ الْأَرْضُ وَالْجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةً وَاحِدَةً ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
فَيَوْمَئِذٍ وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
وَانشَقَّتِ السَّمَاءُ فَهِيَ يَوْمَئِذٍ وَاهِيَةٌ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
وَالْمَلَكُ عَلَىٰ أَرْجَائِهَا ۚ وَيَحْمِلُ عَرْشَ رَبِّكَ فَوْقَهُمْ يَوْمَئِذٍ ثَمَانِيَةٌ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
يَوْمَئِذٍ تُعْرَضُونَ لَا تَخْفَىٰ مِنكُمْ خَافِيَةٌ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ فَيَقُولُ هَاؤُمُ اقْرَءُوا كِتَابِيَهْ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَاقٍ حِسَابِيَهْ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Katika Bustani ya juu,
قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Matunda yake yakaribu.
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا أَسْلَفْتُمْ فِي الْأَيَّامِ الْخَالِيَةِ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِشِمَالِهِ فَيَقُولُ يَا لَيْتَنِي لَمْ أُوتَ كِتَابِيَهْ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيَهْ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
يَا لَيْتَهَا كَانَتِ الْقَاضِيَةَ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
مَا أَغْنَىٰ عَنِّي مَالِيَهْ ۜ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Mali yangu hayakunifaa kitu.
هَلَكَ عَنِّي سُلْطَانِيَهْ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Madaraka yangu yamenipotea.
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
ثُمَّ الْجَحِيمَ صَلُّوهُ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Kisha mtupeni Motoni!
ثُمَّ فِي سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَاسْلُكُوهُ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
إِنَّهُ كَانَ لَا يُؤْمِنُ بِاللَّهِ الْعَظِيمِ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Wala hahimizi kulisha masikini.
فَلَيْسَ لَهُ الْيَوْمَ هَاهُنَا حَمِيمٌ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنْ غِسْلِينٍ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
لَّا يَأْكُلُهُ إِلَّا الْخَاطِئُونَ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
فَلَا أُقْسِمُ بِمَا تُبْصِرُونَ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Basi naapa kwa mnavyo viona,
وَمَا لَا تُبْصِرُونَ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Na msivyo viona,
إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَاعِرٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تُؤْمِنُونَ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
وَلَا بِقَوْلِ كَاهِنٍ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
وَلَوْ تَقَوَّلَ عَلَيْنَا بَعْضَ الْأَقَاوِيلِ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
لَأَخَذْنَا مِنْهُ بِالْيَمِينِ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
ثُمَّ لَقَطَعْنَا مِنْهُ الْوَتِينَ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
فَمَا مِنكُم مِّنْ أَحَدٍ عَنْهُ حَاجِزِينَ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
وَإِنَّهُ لَتَذْكِرَةٌ لِّلْمُتَّقِينَ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
وَإِنَّا لَنَعْلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
وَإِنَّهُ لَحَسْرَةٌ عَلَى الْكَافِرِينَ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
وَإِنَّهُ لَحَقُّ الْيَقِينِ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
← 68 Al-Haqqa (69/114) 70 →
Soma Sura Al-Haqqa kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

69الحاقة Al-Haqqah 📚 52 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema