Sura Adh-Dhariyat kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Adh-Dhariyat na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (60 Aya — مكية). Adh-Dhariyat Sikiliza, Adh-Dhariyat Tafsiri, Adh-Dhariyat mp3, Adh-Dhariyat pdf.

Soma na Sikiliza Sura Adh-Dhariyat

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
وَالذَّارِيَاتِ ذَرْوًا ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
فَالْحَامِلَاتِ وِقْرًا ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Na zinazo beba mizigo,
فَالْجَارِيَاتِ يُسْرًا ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
فَالْمُقَسِّمَاتِ أَمْرًا ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Na zinazo gawanya kwa amri,
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
وَإِنَّ الدِّينَ لَوَاقِعٌ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْحُبُكِ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Naapa kwa mbingu zenye njia,
إِنَّكُمْ لَفِي قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
قُتِلَ الْخَرَّاصُونَ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Wazushi wameangamizwa.
الَّذِينَ هُمْ فِي غَمْرَةٍ سَاهُونَ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Ambao wameghafilika katika ujinga.
يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَسْتَعْجِلُونَ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
وَفِي أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَا أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا ۖ قَالَ سَلَامٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
فَرَاغَ إِلَىٰ أَهْلِهِ فَجَاءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
فَقَرَّبَهُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُهُ فِي صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
قَالُوا كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
۞ قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Tuwatupie mawe ya udongo,
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ الْمُسْلِمِينَ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الْأَلِيمَ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
وَفِي مُوسَىٰ إِذْ أَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
فَأَخَذْنَاهُ وَجُنُودَهُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
وَفِي عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
مَا تَذَرُ مِن شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّىٰ حِينٍ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
فَمَا اسْتَطَاعُوا مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْدٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
وَالْأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
فَفِرُّوا إِلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
وَلَا تَجْعَلُوا مَعَ اللَّهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
كَذَٰلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
أَتَوَاصَوْا بِهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ ۝٥٣
📖 Tafsiri Aya 53
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنتَ بِمَلُومٍ ۝٥٤
📖 Tafsiri Aya 54
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَىٰ تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ ۝٥٥
📖 Tafsiri Aya 55
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ۝٥٦
📖 Tafsiri Aya 56
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ ۝٥٧
📖 Tafsiri Aya 57
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
إِنَّ اللَّهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ ۝٥٨
📖 Tafsiri Aya 58
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ ۝٥٩
📖 Tafsiri Aya 59
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِن يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ ۝٦٠
📖 Tafsiri Aya 60
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
← 50 Adh-Dhariyat (51/114) 52 →
Soma Sura Adh-Dhariyat kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

51الذاريات Adh-Dhariyat 📚 60 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema