Sura Al-'Alaq
19 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
ﮛﮜﮝﮞﮟ
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
ﮠﮡﮢﮣ
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
ﮤﮥﮦﮧ
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
ﮮﮯﮰﮱﯓ
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
ﯔﯕﯖﯗ
Akijiona katajirika.
ﯘﯙﯚﯛﯜ
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
ﯝﯞﯟﯠ
Umemwona yule anaye mkataza
ﯡﯢﯣﯤ
Mja anapo sali?
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
ﯫﯬﯭﯮ
Au anaamrisha uchamngu?
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
ﭣﭤﭥﭦ
Shungi la uwongo, lenye makosa!
ﭧﭨﭩ
Basi na awaite wenzake!
ﭪﭫﭬ
Nasi tutawaita Mazabania!
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema