Sura As-Saffat kwa Kiarabu na Kiswahili
Soma Sura As-Saffat na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (182 Aya — مكية). As-Saffat Sikiliza, As-Saffat Tafsiri, As-Saffat mp3, As-Saffat pdf.Soma na Sikiliza Sura As-Saffat
🎧 Aya
M
Mishary Rashid Alafasy
✓
Mishary Rashid Alafasy
✓
M
Mahmoud Khalil Al-Husary
✓
Mahmoud Khalil Al-Husary
✓
A
Abdurrahman As-Sudais
✓
Abdurrahman As-Sudais
✓
M
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
✓
Mohamed Siddiq Al-Minshawi
✓
A
Abdul Basit Abdul Samad
✓
Abdul Basit Abdul Samad
✓
A
Ali Al-Hudhaify
✓
Ali Al-Hudhaify
✓
A
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
✓
Ahmed ibn Ali al-Ajamy
✓
A
Abu Bakr Ash-Shaatree
✓
Abu Bakr Ash-Shaatree
✓
M
Muhammad Ayyoub
✓
Muhammad Ayyoub
✓
A
Abdullah Basfar
✓
Abdullah Basfar
✓
A
Abdullah Al-Juhani
✓
Abdullah Al-Juhani
✓
M
Maher Al Muaiqly
✓
Maher Al Muaiqly
✓
—
x1
رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ ٥
📖 Tafsiri
Aya 5
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ ٦
📖 Tafsiri
Aya 6
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ ٨
📖 Tafsiri
Aya 8
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ ١٠
📖 Tafsiri
Aya 10
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا ۚ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍ ١١
📖 Tafsiri
Aya 11
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ ١٤
📖 Tafsiri
Aya 14
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
وَقَالُوا إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ ١٥
📖 Tafsiri
Aya 15
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ ١٦
📖 Tafsiri
Aya 16
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ ١٩
📖 Tafsiri
Aya 19
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ الدِّينِ ٢٠
📖 Tafsiri
Aya 20
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ٢١
📖 Tafsiri
Aya 21
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
۞ احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ ٢٢
📖 Tafsiri
Aya 22
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
مِن دُونِ اللَّهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ ٢٣
📖 Tafsiri
Aya 23
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ٢٧
📖 Tafsiri
Aya 27
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ ٢٨
📖 Tafsiri
Aya 28
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
قَالُوا بَل لَّمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ ٢٩
📖 Tafsiri
Aya 29
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَاغِينَ ٣٠
📖 Tafsiri
Aya 30
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا ۖ إِنَّا لَذَائِقُونَ ٣١
📖 Tafsiri
Aya 31
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ ٣٢
📖 Tafsiri
Aya 32
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ ٣٣
📖 Tafsiri
Aya 33
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ ٣٤
📖 Tafsiri
Aya 34
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَٰهَ إِلَّا اللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ ٣٥
📖 Tafsiri
Aya 35
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ ٣٦
📖 Tafsiri
Aya 36
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ ٣٧
📖 Tafsiri
Aya 37
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الْأَلِيمِ ٣٨
📖 Tafsiri
Aya 38
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ٣٩
📖 Tafsiri
Aya 39
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ٤٠
📖 Tafsiri
Aya 40
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ ٤٥
📖 Tafsiri
Aya 45
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ ٤٧
📖 Tafsiri
Aya 47
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ ٤٨
📖 Tafsiri
Aya 48
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ٥٠
📖 Tafsiri
Aya 50
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ ٥١
📖 Tafsiri
Aya 51
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
يَقُولُ أَإِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ ٥٢
📖 Tafsiri
Aya 52
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ ٥٣
📖 Tafsiri
Aya 53
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ ٥٥
📖 Tafsiri
Aya 55
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
قَالَ تَاللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ ٥٦
📖 Tafsiri
Aya 56
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ ٥٧
📖 Tafsiri
Aya 57
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
إِلَّا مَوْتَتَنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ ٥٩
📖 Tafsiri
Aya 59
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ٦٠
📖 Tafsiri
Aya 60
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ ٦١
📖 Tafsiri
Aya 61
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ ٦٢
📖 Tafsiri
Aya 62
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ ٦٣
📖 Tafsiri
Aya 63
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ ٦٤
📖 Tafsiri
Aya 64
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ ٦٥
📖 Tafsiri
Aya 65
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ ٦٦
📖 Tafsiri
Aya 66
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ ٦٧
📖 Tafsiri
Aya 67
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ ٦٨
📖 Tafsiri
Aya 68
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
فَهُمْ عَلَىٰ آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ ٧٠
📖 Tafsiri
Aya 70
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الْأَوَّلِينَ ٧١
📖 Tafsiri
Aya 71
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ ٧٣
📖 Tafsiri
Aya 73
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ٧٤
📖 Tafsiri
Aya 74
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
وَلَقَدْ نَادَانَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ ٧٥
📖 Tafsiri
Aya 75
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
وَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ ٧٦
📖 Tafsiri
Aya 76
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُ هُمُ الْبَاقِينَ ٧٧
📖 Tafsiri
Aya 77
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ٧٨
📖 Tafsiri
Aya 78
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ٨٠
📖 Tafsiri
Aya 80
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ٨١
📖 Tafsiri
Aya 81
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِ لَإِبْرَاهِيمَ ٨٣
📖 Tafsiri
Aya 83
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَاذَا تَعْبُدُونَ ٨٥
📖 Tafsiri
Aya 85
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
أَئِفْكًا آلِهَةً دُونَ اللَّهِ تُرِيدُونَ ٨٦
📖 Tafsiri
Aya 86
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ٨٧
📖 Tafsiri
Aya 87
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
فَرَاغَ إِلَىٰ آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ ٩١
📖 Tafsiri
Aya 91
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًا بِالْيَمِينِ ٩٣
📖 Tafsiri
Aya 93
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ ٩٥
📖 Tafsiri
Aya 95
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
وَاللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ ٩٦
📖 Tafsiri
Aya 96
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
قَالُوا ابْنُوا لَهُ بُنْيَانًا فَأَلْقُوهُ فِي الْجَحِيمِ ٩٧
📖 Tafsiri
Aya 97
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
فَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَسْفَلِينَ ٩٨
📖 Tafsiri
Aya 98
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ ٩٩
📖 Tafsiri
Aya 99
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ ١٠٠
📖 Tafsiri
Aya 100
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ ١٠٢
📖 Tafsiri
Aya 102
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ ١٠٣
📖 Tafsiri
Aya 103
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ١٠٥
📖 Tafsiri
Aya 105
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ ١٠٦
📖 Tafsiri
Aya 106
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ١٠٨
📖 Tafsiri
Aya 108
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ١١٠
📖 Tafsiri
Aya 110
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ١١١
📖 Tafsiri
Aya 111
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ ١١٢
📖 Tafsiri
Aya 112
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ ١١٣
📖 Tafsiri
Aya 113
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ١١٤
📖 Tafsiri
Aya 114
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ ١١٥
📖 Tafsiri
Aya 115
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ ١١٦
📖 Tafsiri
Aya 116
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ ١١٧
📖 Tafsiri
Aya 117
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
وَهَدَيْنَاهُمَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ ١١٨
📖 Tafsiri
Aya 118
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِي الْآخِرِينَ ١١٩
📖 Tafsiri
Aya 119
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ١٢١
📖 Tafsiri
Aya 121
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ١٢٢
📖 Tafsiri
Aya 122
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ١٢٣
📖 Tafsiri
Aya 123
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ الْخَالِقِينَ ١٢٥
📖 Tafsiri
Aya 125
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
اللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ ١٢٦
📖 Tafsiri
Aya 126
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ١٢٧
📖 Tafsiri
Aya 127
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ١٢٨
📖 Tafsiri
Aya 128
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ١٢٩
📖 Tafsiri
Aya 129
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ١٣١
📖 Tafsiri
Aya 131
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ١٣٢
📖 Tafsiri
Aya 132
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ الْمُرْسَلِينَ ١٣٣
📖 Tafsiri
Aya 133
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
إِذْ نَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ ١٣٤
📖 Tafsiri
Aya 134
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ ١٣٥
📖 Tafsiri
Aya 135
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ ١٣٧
📖 Tafsiri
Aya 137
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ١٣٩
📖 Tafsiri
Aya 139
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
إِذْ أَبَقَ إِلَى الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ١٤٠
📖 Tafsiri
Aya 140
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ الْمُدْحَضِينَ ١٤١
📖 Tafsiri
Aya 141
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
فَالْتَقَمَهُ الْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ ١٤٢
📖 Tafsiri
Aya 142
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
فَلَوْلَا أَنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُسَبِّحِينَ ١٤٣
📖 Tafsiri
Aya 143
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
لَلَبِثَ فِي بَطْنِهِ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ١٤٤
📖 Tafsiri
Aya 144
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
۞ فَنَبَذْنَاهُ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ سَقِيمٌ ١٤٥
📖 Tafsiri
Aya 145
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
وَأَنبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ ١٤٦
📖 Tafsiri
Aya 146
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
وَأَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ مِائَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ ١٤٧
📖 Tafsiri
Aya 147
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
فَآمَنُوا فَمَتَّعْنَاهُمْ إِلَىٰ حِينٍ ١٤٨
📖 Tafsiri
Aya 148
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
فَاسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ الْبَنَاتُ وَلَهُمُ الْبَنُونَ ١٤٩
📖 Tafsiri
Aya 149
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
أَمْ خَلَقْنَا الْمَلَائِكَةَ إِنَاثًا وَهُمْ شَاهِدُونَ ١٥٠
📖 Tafsiri
Aya 150
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
أَلَا إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ ١٥١
📖 Tafsiri
Aya 151
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
وَلَدَ اللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ١٥٢
📖 Tafsiri
Aya 152
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
أَصْطَفَى الْبَنَاتِ عَلَى الْبَنِينَ ١٥٣
📖 Tafsiri
Aya 153
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
فَأْتُوا بِكِتَابِكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ١٥٧
📖 Tafsiri
Aya 157
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
وَجَعَلُوا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ الْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ١٥٨
📖 Tafsiri
Aya 158
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ ١٥٩
📖 Tafsiri
Aya 159
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ١٦٠
📖 Tafsiri
Aya 160
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ ١٦٤
📖 Tafsiri
Aya 164
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ ١٦٥
📖 Tafsiri
Aya 165
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ ١٦٦
📖 Tafsiri
Aya 166
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ الْأَوَّلِينَ ١٦٨
📖 Tafsiri
Aya 168
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
لَكُنَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ١٦٩
📖 Tafsiri
Aya 169
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا الْمُرْسَلِينَ ١٧١
📖 Tafsiri
Aya 171
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
إِنَّهُمْ لَهُمُ الْمَنصُورُونَ ١٧٢
📖 Tafsiri
Aya 172
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ الْغَالِبُونَ ١٧٣
📖 Tafsiri
Aya 173
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَاءَ صَبَاحُ الْمُنذَرِينَ ١٧٧
📖 Tafsiri
Aya 177
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ ١٨٠
📖 Tafsiri
Aya 180
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
وَالْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ١٨٢
📖 Tafsiri
Aya 182
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Soma Sura As-Saffat kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema

