Sura As-Saffat kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura As-Saffat na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (182 Aya — مكية). As-Saffat Sikiliza, As-Saffat Tafsiri, As-Saffat mp3, As-Saffat pdf.

Soma na Sikiliza Sura As-Saffat

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
وَالصَّافَّاتِ صَفًّا ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرًا ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Na kwa wenye kukataza mabaya.
فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرًا ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَانٍ مَّارِدٍ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا ۚ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
وَإِذَا ذُكِّرُوا لَا يَذْكُرُونَ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
وَقَالُوا إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Hata baba zetu wa zamani?
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَاخِرُونَ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ الدِّينِ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
۞ احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
مِن دُونِ اللَّهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْئُولُونَ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Bali hii leo, watasalimu amri.
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
قَالُوا بَل لَّمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَاغِينَ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا ۖ إِنَّا لَذَائِقُونَ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَٰهَ إِلَّا اللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الْأَلِيمِ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
أُولَٰئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
فَوَاكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Matunda, nao watahishimiwa.
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Katika Bustani za neema.
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Wako juu ya viti wamekabiliana.
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
بَيْضَاءَ لَذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
يَقُولُ أَإِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ ۝٥٣
📖 Tafsiri Aya 53
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ ۝٥٤
📖 Tafsiri Aya 54
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ ۝٥٥
📖 Tafsiri Aya 55
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
قَالَ تَاللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ ۝٥٦
📖 Tafsiri Aya 56
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ ۝٥٧
📖 Tafsiri Aya 57
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ ۝٥٨
📖 Tafsiri Aya 58
Je! Sisi hatutakufa,
إِلَّا مَوْتَتَنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ ۝٥٩
📖 Tafsiri Aya 59
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ۝٦٠
📖 Tafsiri Aya 60
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ ۝٦١
📖 Tafsiri Aya 61
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ ۝٦٢
📖 Tafsiri Aya 62
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ ۝٦٣
📖 Tafsiri Aya 63
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ ۝٦٤
📖 Tafsiri Aya 64
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ ۝٦٥
📖 Tafsiri Aya 65
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ ۝٦٦
📖 Tafsiri Aya 66
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ ۝٦٧
📖 Tafsiri Aya 67
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ ۝٦٨
📖 Tafsiri Aya 68
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا آبَاءَهُمْ ضَالِّينَ ۝٦٩
📖 Tafsiri Aya 69
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
فَهُمْ عَلَىٰ آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ ۝٧٠
📖 Tafsiri Aya 70
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الْأَوَّلِينَ ۝٧١
📖 Tafsiri Aya 71
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ ۝٧٢
📖 Tafsiri Aya 72
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ ۝٧٣
📖 Tafsiri Aya 73
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ۝٧٤
📖 Tafsiri Aya 74
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
وَلَقَدْ نَادَانَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ ۝٧٥
📖 Tafsiri Aya 75
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
وَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ ۝٧٦
📖 Tafsiri Aya 76
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُ هُمُ الْبَاقِينَ ۝٧٧
📖 Tafsiri Aya 77
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ۝٧٨
📖 Tafsiri Aya 78
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي الْعَالَمِينَ ۝٧٩
📖 Tafsiri Aya 79
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ۝٨٠
📖 Tafsiri Aya 80
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ۝٨١
📖 Tafsiri Aya 81
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ ۝٨٢
📖 Tafsiri Aya 82
Kisha tukawazamisha wale wengine.
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِ لَإِبْرَاهِيمَ ۝٨٣
📖 Tafsiri Aya 83
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
إِذْ جَاءَ رَبَّهُ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ۝٨٤
📖 Tafsiri Aya 84
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَاذَا تَعْبُدُونَ ۝٨٥
📖 Tafsiri Aya 85
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
أَئِفْكًا آلِهَةً دُونَ اللَّهِ تُرِيدُونَ ۝٨٦
📖 Tafsiri Aya 86
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ۝٨٧
📖 Tafsiri Aya 87
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِي النُّجُومِ ۝٨٨
📖 Tafsiri Aya 88
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٌ ۝٨٩
📖 Tafsiri Aya 89
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
فَتَوَلَّوْا عَنْهُ مُدْبِرِينَ ۝٩٠
📖 Tafsiri Aya 90
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
فَرَاغَ إِلَىٰ آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ ۝٩١
📖 Tafsiri Aya 91
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ ۝٩٢
📖 Tafsiri Aya 92
Mna nini hata hamsemi?
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًا بِالْيَمِينِ ۝٩٣
📖 Tafsiri Aya 93
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
فَأَقْبَلُوا إِلَيْهِ يَزِفُّونَ ۝٩٤
📖 Tafsiri Aya 94
Basi wakamjia upesi upesi.
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ ۝٩٥
📖 Tafsiri Aya 95
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
وَاللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ ۝٩٦
📖 Tafsiri Aya 96
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
قَالُوا ابْنُوا لَهُ بُنْيَانًا فَأَلْقُوهُ فِي الْجَحِيمِ ۝٩٧
📖 Tafsiri Aya 97
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
فَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَسْفَلِينَ ۝٩٨
📖 Tafsiri Aya 98
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ ۝٩٩
📖 Tafsiri Aya 99
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ ۝١٠٠
📖 Tafsiri Aya 100
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ ۝١٠١
📖 Tafsiri Aya 101
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ ۝١٠٢
📖 Tafsiri Aya 102
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ ۝١٠٣
📖 Tafsiri Aya 103
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
وَنَادَيْنَاهُ أَن يَا إِبْرَاهِيمُ ۝١٠٤
📖 Tafsiri Aya 104
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ۝١٠٥
📖 Tafsiri Aya 105
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ ۝١٠٦
📖 Tafsiri Aya 106
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ ۝١٠٧
📖 Tafsiri Aya 107
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ۝١٠٨
📖 Tafsiri Aya 108
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ ۝١٠٩
📖 Tafsiri Aya 109
Iwe salama kwa Ibrahim!
كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ۝١١٠
📖 Tafsiri Aya 110
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ۝١١١
📖 Tafsiri Aya 111
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ ۝١١٢
📖 Tafsiri Aya 112
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ ۝١١٣
📖 Tafsiri Aya 113
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ۝١١٤
📖 Tafsiri Aya 114
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ ۝١١٥
📖 Tafsiri Aya 115
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ ۝١١٦
📖 Tafsiri Aya 116
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ ۝١١٧
📖 Tafsiri Aya 117
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
وَهَدَيْنَاهُمَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ ۝١١٨
📖 Tafsiri Aya 118
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِي الْآخِرِينَ ۝١١٩
📖 Tafsiri Aya 119
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ۝١٢٠
📖 Tafsiri Aya 120
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ۝١٢١
📖 Tafsiri Aya 121
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ۝١٢٢
📖 Tafsiri Aya 122
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ۝١٢٣
📖 Tafsiri Aya 123
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ أَلَا تَتَّقُونَ ۝١٢٤
📖 Tafsiri Aya 124
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ الْخَالِقِينَ ۝١٢٥
📖 Tafsiri Aya 125
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
اللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ ۝١٢٦
📖 Tafsiri Aya 126
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ۝١٢٧
📖 Tafsiri Aya 127
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ۝١٢٨
📖 Tafsiri Aya 128
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ۝١٢٩
📖 Tafsiri Aya 129
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ إِلْ يَاسِينَ ۝١٣٠
📖 Tafsiri Aya 130
Iwe salama kwa Ilyas.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ۝١٣١
📖 Tafsiri Aya 131
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ۝١٣٢
📖 Tafsiri Aya 132
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ الْمُرْسَلِينَ ۝١٣٣
📖 Tafsiri Aya 133
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
إِذْ نَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ ۝١٣٤
📖 Tafsiri Aya 134
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ ۝١٣٥
📖 Tafsiri Aya 135
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ ۝١٣٦
📖 Tafsiri Aya 136
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ ۝١٣٧
📖 Tafsiri Aya 137
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
وَبِاللَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ۝١٣٨
📖 Tafsiri Aya 138
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ۝١٣٩
📖 Tafsiri Aya 139
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
إِذْ أَبَقَ إِلَى الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ۝١٤٠
📖 Tafsiri Aya 140
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ الْمُدْحَضِينَ ۝١٤١
📖 Tafsiri Aya 141
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
فَالْتَقَمَهُ الْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ ۝١٤٢
📖 Tafsiri Aya 142
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
فَلَوْلَا أَنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُسَبِّحِينَ ۝١٤٣
📖 Tafsiri Aya 143
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
لَلَبِثَ فِي بَطْنِهِ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ۝١٤٤
📖 Tafsiri Aya 144
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
۞ فَنَبَذْنَاهُ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ سَقِيمٌ ۝١٤٥
📖 Tafsiri Aya 145
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
وَأَنبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ ۝١٤٦
📖 Tafsiri Aya 146
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
وَأَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ مِائَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ ۝١٤٧
📖 Tafsiri Aya 147
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
فَآمَنُوا فَمَتَّعْنَاهُمْ إِلَىٰ حِينٍ ۝١٤٨
📖 Tafsiri Aya 148
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
فَاسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ الْبَنَاتُ وَلَهُمُ الْبَنُونَ ۝١٤٩
📖 Tafsiri Aya 149
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
أَمْ خَلَقْنَا الْمَلَائِكَةَ إِنَاثًا وَهُمْ شَاهِدُونَ ۝١٥٠
📖 Tafsiri Aya 150
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
أَلَا إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ ۝١٥١
📖 Tafsiri Aya 151
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
وَلَدَ اللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ۝١٥٢
📖 Tafsiri Aya 152
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
أَصْطَفَى الْبَنَاتِ عَلَى الْبَنِينَ ۝١٥٣
📖 Tafsiri Aya 153
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ ۝١٥٤
📖 Tafsiri Aya 154
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ ۝١٥٥
📖 Tafsiri Aya 155
Hamkumbuki?
أَمْ لَكُمْ سُلْطَانٌ مُّبِينٌ ۝١٥٦
📖 Tafsiri Aya 156
Au mnayo hoja iliyo wazi?
فَأْتُوا بِكِتَابِكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ۝١٥٧
📖 Tafsiri Aya 157
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
وَجَعَلُوا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ الْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ۝١٥٨
📖 Tafsiri Aya 158
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ ۝١٥٩
📖 Tafsiri Aya 159
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ۝١٦٠
📖 Tafsiri Aya 160
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ ۝١٦١
📖 Tafsiri Aya 161
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
مَا أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَاتِنِينَ ۝١٦٢
📖 Tafsiri Aya 162
Hamwezi kuwapoteza
إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ الْجَحِيمِ ۝١٦٣
📖 Tafsiri Aya 163
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ ۝١٦٤
📖 Tafsiri Aya 164
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ ۝١٦٥
📖 Tafsiri Aya 165
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ ۝١٦٦
📖 Tafsiri Aya 166
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
وَإِن كَانُوا لَيَقُولُونَ ۝١٦٧
📖 Tafsiri Aya 167
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ الْأَوَّلِينَ ۝١٦٨
📖 Tafsiri Aya 168
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
لَكُنَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ۝١٦٩
📖 Tafsiri Aya 169
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
فَكَفَرُوا بِهِ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ ۝١٧٠
📖 Tafsiri Aya 170
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا الْمُرْسَلِينَ ۝١٧١
📖 Tafsiri Aya 171
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
إِنَّهُمْ لَهُمُ الْمَنصُورُونَ ۝١٧٢
📖 Tafsiri Aya 172
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ الْغَالِبُونَ ۝١٧٣
📖 Tafsiri Aya 173
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ ۝١٧٤
📖 Tafsiri Aya 174
Basi waachilie mbali kwa muda.
وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ ۝١٧٥
📖 Tafsiri Aya 175
Na watazame, nao wataona.
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ ۝١٧٦
📖 Tafsiri Aya 176
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَاءَ صَبَاحُ الْمُنذَرِينَ ۝١٧٧
📖 Tafsiri Aya 177
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ ۝١٧٨
📖 Tafsiri Aya 178
Na waache kwa muda.
وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ ۝١٧٩
📖 Tafsiri Aya 179
Na tazama, na wao wataona.
سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ ۝١٨٠
📖 Tafsiri Aya 180
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
وَسَلَامٌ عَلَى الْمُرْسَلِينَ ۝١٨١
📖 Tafsiri Aya 181
Na Salamu juu ya Mitume.
وَالْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ۝١٨٢
📖 Tafsiri Aya 182
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
← 36 As-Saffat (37/114) 38 →
Soma Sura As-Saffat kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

37الصافات As-Saffat 📚 182 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema