| وَالصَّافَّاتِ صَفًّا(1) Naapa kwa wanao jipanga kwa safu. | 
| فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرًا(2) Na kwa wenye kukataza mabaya. | 
| فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرًا(3) Na kwa wenye kusoma Ukumbusho. | 
| إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ(4) Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. | 
| رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ(5) Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote. | 
| إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ(6) Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota. | 
| وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَانٍ مَّارِدٍ(7) Na kulinda na kila shet'ani a'si. | 
| لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ(8) Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande. | 
| دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ(9) Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu. | 
| إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ(10) Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara. | 
| فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا ۚ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍ(11) Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata. | 
| بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ(12) Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara. | 
| وَإِذَا ذُكِّرُوا لَا يَذْكُرُونَ(13) Na wanapo kumbushwa hawakumbuki. | 
| وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ(14) Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara. | 
| وَقَالُوا إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ(15) Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri. | 
| أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ(16) Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa? | 
| أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ(17) Hata baba zetu wa zamani? | 
| قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَاخِرُونَ(18) Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili. | 
| فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ(19) Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona! | 
| وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ الدِّينِ(20) Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo. | 
| هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ(21) Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha. | 
| ۞ احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ(22) Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu - | 
| مِن دُونِ اللَّهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ(23) Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu! | 
| وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْئُولُونَ(24) Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa: | 
| مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ(25) Mna nini? Mbona hamsaidiani? | 
| بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ(26) Bali hii leo, watasalimu amri. | 
| وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ(27) Watakabiliana wao kwa wao kuulizana. | 
| قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ(28) Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia. | 
| قَالُوا بَل لَّمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ(29) Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini. | 
| وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَاغِينَ(30) Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu. | 
| فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا ۖ إِنَّا لَذَائِقُونَ(31) Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu. | 
| فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ(32) Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu. | 
| فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ(33) Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja. | 
| إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ(34) Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu. | 
| إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَٰهَ إِلَّا اللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ(35) Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna. | 
| وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ(36) Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu? | 
| بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ(37) Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume. | 
| إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الْأَلِيمِ(38) Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu. | 
| وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ(39) Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya. | 
| إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ(40) Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. | 
| أُولَٰئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ(41) Hao ndio watakao pata riziki maalumu, | 
| فَوَاكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ(42) Matunda, nao watahishimiwa. | 
| فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ(43) Katika Bustani za neema. | 
| عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ(44) Wako juu ya viti wamekabiliana. | 
| يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ(45) Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem | 
| بَيْضَاءَ لَذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ(46) Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao. | 
| لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ(47) Hakina madhara, wala hakiwaleweshi. | 
| وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ(48) Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri. | 
| كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ(49) Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika. | 
| فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ(50) Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe. | 
| قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ(51) Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki | 
| يَقُولُ أَإِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ(52) Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki | 
| أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ(53) Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa? | 
| قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ(54) Atasema: Je! Nyie mnawaona? | 
| فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ(55) Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu. | 
| قَالَ تَاللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ(56) Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza. | 
| وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ(57) Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa. | 
| أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ(58) Je! Sisi hatutakufa, | 
| إِلَّا مَوْتَتَنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ(59) Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa. | 
| إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ(60) Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa. | 
| لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ(61) Kwa mfano wa haya nawatende watendao. | 
| أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ(62) Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum? | 
| إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ(63) Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu. | 
| إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ(64) Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu. | 
| طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ(65) Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani. | 
| فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ(66) Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo. | 
| ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ(67) Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka. | 
| ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ(68) Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu. | 
| إِنَّهُمْ أَلْفَوْا آبَاءَهُمْ ضَالِّينَ(69) Hakika waliwakuta baba zao wamepotea. | 
| فَهُمْ عَلَىٰ آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ(70) Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao. | 
| وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الْأَوَّلِينَ(71) Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani. | 
| وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ(72) Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji. | 
| فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ(73) Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa. | 
| إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ(74) Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. | 
| وَلَقَدْ نَادَانَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ(75) Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji. | 
| وَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ(76) Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa. | 
| وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُ هُمُ الْبَاقِينَ(77) Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia. | 
| وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ(78) Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye. | 
| سَلَامٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي الْعَالَمِينَ(79) Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote! | 
| إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ(80) Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. | 
| إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ(81) Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. | 
| ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ(82) Kisha tukawazamisha wale wengine. | 
| ۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِ لَإِبْرَاهِيمَ(83) Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake, | 
| إِذْ جَاءَ رَبَّهُ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ(84) Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima. | 
| إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَاذَا تَعْبُدُونَ(85) Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini? | 
| أَئِفْكًا آلِهَةً دُونَ اللَّهِ تُرِيدُونَ(86) Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu? | 
| فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ(87) Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote? | 
| فَنَظَرَ نَظْرَةً فِي النُّجُومِ(88) Kisha akapiga jicho kutazama nyota. | 
| فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٌ(89) Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa! | 
| فَتَوَلَّوْا عَنْهُ مُدْبِرِينَ(90) Nao wakamwacha, wakampa kisogo. | 
| فَرَاغَ إِلَىٰ آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ(91) Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli? | 
| مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ(92) Mna nini hata hamsemi? | 
| فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًا بِالْيَمِينِ(93) Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia. | 
| فَأَقْبَلُوا إِلَيْهِ يَزِفُّونَ(94) Basi wakamjia upesi upesi. | 
| قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ(95) Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe? | 
| وَاللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ(96) Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya! | 
| قَالُوا ابْنُوا لَهُ بُنْيَانًا فَأَلْقُوهُ فِي الْجَحِيمِ(97) Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo! | 
| فَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَسْفَلِينَ(98) Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini. | 
| وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ(99) Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa. | 
| رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ(100) Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema. | 
| فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ(101) Basi tukambashiria mwana aliye mpole. | 
| فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ(102) Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri. | 
| فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ(103) Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji. | 
| وَنَادَيْنَاهُ أَن يَا إِبْرَاهِيمُ(104) Tulimwita: Ewe Ibrahim! | 
| قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ(105) Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema. | 
| إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ(106) Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri. | 
| وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ(107) Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu. | 
| وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ(108) Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye. | 
| سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ(109) Iwe salama kwa Ibrahim! | 
| كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ(110) Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. | 
| إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ(111) Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. | 
| وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ(112) Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema. | 
| وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ(113) Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi. | 
| وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ(114) Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni. | 
| وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ(115) Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa. | 
| وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ(116) Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda. | 
| وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ(117) Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha. | 
| وَهَدَيْنَاهُمَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ(118) Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka. | 
| وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِي الْآخِرِينَ(119) Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye. | 
| سَلَامٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ(120) Iwe salama kwa Musa na Haruni! | 
| إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ(121) Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. | 
| إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ(122) Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini. | 
| وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ(123) Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume. | 
| إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ أَلَا تَتَّقُونَ(124) Alipo waambia watu wake: Hamwogopi? | 
| أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ الْخَالِقِينَ(125) Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji, | 
| اللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ(126) Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani? | 
| فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ(127) Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa; | 
| إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ(128) Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. | 
| وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ(129) Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye. | 
| سَلَامٌ عَلَىٰ إِلْ يَاسِينَ(130) Iwe salama kwa Ilyas. | 
| إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ(131) Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema. | 
| إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ(132) Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini. | 
| وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ الْمُرْسَلِينَ(133) Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume. | 
| إِذْ نَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ(134) Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote, | 
| إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ(135) Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma. | 
| ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ(136) Kisha tukawaangamiza wale wengineo. | 
| وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ(137) Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi, | 
| وَبِاللَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ(138) Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini? | 
| وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ(139) Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume. | 
| إِذْ أَبَقَ إِلَى الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ(140) Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni. | 
| فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ الْمُدْحَضِينَ(141) Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa. | 
| فَالْتَقَمَهُ الْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ(142) Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. | 
| فَلَوْلَا أَنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُسَبِّحِينَ(143) Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu, | 
| لَلَبِثَ فِي بَطْنِهِ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ(144) Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa. | 
| ۞ فَنَبَذْنَاهُ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ سَقِيمٌ(145) Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa. | 
| وَأَنبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ(146) Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye. | 
| وَأَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ مِائَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ(147) Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi. | 
| فَآمَنُوا فَمَتَّعْنَاهُمْ إِلَىٰ حِينٍ(148) Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda. | 
| فَاسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ الْبَنَاتُ وَلَهُمُ الْبَنُونَ(149) Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume? | 
| أَمْ خَلَقْنَا الْمَلَائِكَةَ إِنَاثًا وَهُمْ شَاهِدُونَ(150) Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia? | 
| أَلَا إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ(151) Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema: | 
| وَلَدَ اللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ(152) Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo! | 
| أَصْطَفَى الْبَنَاتِ عَلَى الْبَنِينَ(153) Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume? | 
| مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ(154) Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi? | 
| أَفَلَا تَذَكَّرُونَ(155) Hamkumbuki? | 
| أَمْ لَكُمْ سُلْطَانٌ مُّبِينٌ(156) Au mnayo hoja iliyo wazi? | 
| فَأْتُوا بِكِتَابِكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ(157) Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli. | 
| وَجَعَلُوا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ الْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ(158) Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa. | 
| سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ(159) Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia. | 
| إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ(160) Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. | 
| فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ(161) Basi hakika nyinyi na mnao waabudu | 
| مَا أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَاتِنِينَ(162) Hamwezi kuwapoteza | 
| إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ الْجَحِيمِ(163) Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni. | 
| وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ(164) Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu. | 
| وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ(165) Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu. | 
| وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ(166) Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa. | 
| وَإِن كَانُوا لَيَقُولُونَ(167) Na walikuwapo walio kuwa wakisema: | 
| لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ الْأَوَّلِينَ(168) Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani, | 
| لَكُنَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ(169) Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi. | 
| فَكَفَرُوا بِهِ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ(170) Lakini waliukataa. Basi watakuja jua. | 
| وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا الْمُرْسَلِينَ(171) Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa. | 
| إِنَّهُمْ لَهُمُ الْمَنصُورُونَ(172) Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa. | 
| وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ الْغَالِبُونَ(173) Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda. | 
| فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ(174) Basi waachilie mbali kwa muda. | 
| وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ(175) Na watazame, nao wataona. | 
| أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ(176) Je! Wanaihimiza adhabu yetu? | 
| فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَاءَ صَبَاحُ الْمُنذَرِينَ(177) Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa. | 
| وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ(178) Na waache kwa muda. | 
| وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ(179) Na tazama, na wao wataona. | 
| سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ(180) Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia. | 
| وَسَلَامٌ عَلَى الْمُرْسَلِينَ(181) Na Salamu juu ya Mitume. | 
| وَالْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ(182) Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. |